MOTO WA BURUDANI KUWAKA COCO BEACH MWAKA MPYA

Wapenzi wa burudani  ya muziki wa kizazi kipya  watapata burudani ya fungua mwaka kutoka kwa magwiji wa muziki wa kizazi kipya ambao wanatamba nchini katika tamasha la  wazi la maisha murua na Vodacom katika ufukwe wa Coco beach jijini Dar es Salaam.Baadhi ya magwiji hao ni Profesa J,Temba,Chege,Roma Mkatoliki na wengineo wengi.

Tamasha hili  litakalokutanisha magwiji wa bongo fleva ambalo limeanza kuwa gumzo la  jiji kutokana na kuwa na burudani za aina mbalimbali kwa ajili ya kukonga nyoyo za wapenzi wa burudani  limeandaliwa na Vodacom Tanzania.

Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu amesema kuwa Vodacom imeamua kuandaa tamasha hili la”Vodacom Maisha ni Murua” kwa ajili ya kuwapatia furaha na burudani wateja wake na  wananchi kwa ujumla katika sikukuu ya  mwaka mpya vilevile wananchi watapata fursa ya kujinunulia bidhaa mbalimbali za huduma za Mawasiliano kwa gharama nafuu.

“Kama ilivyo kauli mbiu yetu kuwa “Ukiwa na Vodacom maisha ni murua”tunahakikisha mbali na kutoa huduma bora kwa wateja wetu pia tunajua kuwa kuna muda wanahitaji kufurahi kwa burudani  hivyo ndio maana tunaandaa na kudhamini matamasha ya  aina hii na tutaendelea kufanya hivyo siku zote ikiwa ni moja ya njia ya kusema ahsante kwa wateja wetu kwa kutuunga mkono”Alisema.

Alisema mwaka huu burudani kupitia matamasha haya imekuwa jijini Dar es salaam  wakati mikakati inafanyika kuhakikisha burudani hii inasambazwa kwa wateja wote nchi nzima “Tunawajali na kuwasikiliza wateja wetu ambao kwetu ni wafalme hivyo tutahakikisha huduma bora na burudani katika kipindi maalum kama hiki inawafikia katika siku za usoni”.Alisema Nkurlu.

Post a Comment

Previous Post Next Post