REA kuipatia umeme shule ya Chief Hangaya iliyopo Magu.

 

Mkuu wa Wilaya ya Magu, Mhe. Rachel Kasanda (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Mhe, Janet Mbene (wa tatu-kulia), baada ya kikao kifupi kujadili utekelezaji wa miradi ya nishati vijijini Septemba 6, 2023. Wengine kutoka kushoto ni Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Mwanza Mhandisi Ernest Makale, Wajumbe wa Bodi Florian Haule na Mhandisi Styden Rwebangila pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi Romanus Lwena.

Veronica Simba – REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeahidi kugharamia gharama zote za kuunganisha umeme katika Shule ya Msingi ya Chifu Hangaya wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza, inayojengwa kwa ufadhili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ikumbukwe Rais Samia alisimikwa kuwa Chifu Mkuu wa Machifu Tanzania wakati wa Hafla iliyofanyika Agosti 8, 2021 katika Viwanja vya Red Cross eneo la Kisesa, wilayani Magu na kupewa jina la Chifu Hangaya hivyo shule hiyo imepewa jina lake.


Post a Comment

Previous Post Next Post