-Waziri Mavunde aingia mtaani na kikosi kazi kwenye eneo la maficho
-Aupongeza Uongozi wa Mkoa na Vyombo vya Usalama Mbeya
-Aagiza kusimamisha Leseni za biashara ya Madini za watuhumiwa
-Dhahabu iliyokamatwa ina thamani ya Tsh 1,555,476,586
-Serikali ingepata mapato ya Tsh 144,659,322
Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linawashikilia wafanyabiashara wa madini 10 kwa tuhuma za utoroshaji wa madini Kilogramu 9.8 yenye thamani ya Tsh 1,555,476,586.
Akitoa taarifa hiyo kwa wanahabari,Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amesema wafanyabiashara hao walikamatwa siku ya Jumamosi saa 10:27 Alfajiri Katika mtaa wa Ilomba Jijini Mbeya kwenye nyumba waliyokuwa wamepanga wakiwa na vipande 344 ya dhahabu iliyochomwa yenye uzito wa Kilogramu 9.8 pamoja na vifaa mbalimbali kama vile Precious Metal analayzer (XRF) aina ya Niton DXL thermoscientific, mitungi ya gesi, jiko na vyungu kwa ajili ya kuchomea dhahabu, Kipimo cha maji cha kupimia dhahabu, mizani kadhaa pamoja na kemikali aina ya borax.
Waziri Mavunde ametoa rai kwa wafanyabiashara wote wa madini kuhakikisha wanazingatia sheria na kanuni za kufanya biashara ya madini nchini na wote watakaobainika kutorosha madini watachukuliwa hatua za kisheria pamoja na kufutiwa Leseni zao.
Aidha Waziri Mavunde ameagiza kusimamishwa kwa Leseni za biashara ya Madini za watuhumiwa nchi nzima wakati taratibu za upepelezi zikiendelea kabla ya kufikishwa Mahakamani.
Post a Comment