Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde ameanza ujenzi wa viwanja vya michezo ya mpira wa kikapu(basketball),mpira wa pete(netball) na mpira wa wavu(volleyball) katika eneo la shule ya Sekondar Kiwanja cha Ndege Jijini Dodoma.
Ujenzi huu unatokana na ahadi ambayo Mbunge Mavunde aliitoa wakati wa mahafali ya wanafunzi wa kidato cha IV alipokuwa Mgeni Rasmi.
Pamoja na ujenzi huo,Mbunge Mavunde ameahidi kuweka taa katika uwanja huo ili uwe unatumika muda wote,kugawa seti za michezo na kununua tanki la kuhifadhi maji.
Akitoa taarifa ya maendeleo ya shule,Mkuu wa Shule Sekondari Kiwanja cha Ndege Ndg. Daniel ameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Mh Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa madarasa na fedha Tsh 50,000,000 za umaliziaji ujenzi wa maabara na kuongeza pia kukamilika kwa ujenzi wa michezo hapo shuleni utasaidia kuimarisha afya za wanafunzi na kukuza vipaji vyao kupitia michezo.
Post a Comment