Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amenuia kufanya maboresho makubwa kwa kushirikiana na Jiji la Dodoma kwa lengo la kuinua elimu Jijini hapo ambapo moja ya maeneo ambayo ameyapa kipaumbele ni ununuzi wa mashine(photocopiers)kubwa 10 na kugawa kwenye Tarafa ili kuwezesha uchapishaji mitihani ya majaribio ya kila wiki na hivyo kupunguza gharama za uandaaji wa mitihani.
Ni imani yetu kwamba kupitia juhudi hizi na za serikali taaluma ndani ya Dodoma Jiji itaendelea kukua na kuwafanya wanafunzi kufanya vizuri zaidi na kupata uelewa wa kutosha.Ili kupata nafasi ya kupanga mikakati vizuri,kuanzia mwaka huu nitaanzisha Teachers’ Breakfast Meeting ambapo viongozi tutakuwa tunakutana na walimu wote na wadau wa elimu mara mbili kwa mwaka kujipanga kuboresha elimu Jijini Dodoma”Alisema Mavunde
Akitoa shukrani,Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Ndg. John Lipesi Kayombo ameishukuru TFF na NBS kwa michango yao ya mipira na chaki ambayo itasaidia kukuza michezo na kuongeza ufanisi wa ufundishaji katika Jiji la Dodoma.
Post a Comment