Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa akizungumza na waandishi wa habari wa mitandaoni na bloga Desemba 18, 2025 jijini Dar es Salaam.
...............................
Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
KATIBU Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na
Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amewataka waandishi wa habari wa mtandaoni kukabiliana na watu wanaowaita ni
dhaifu katika kufanya kazi zao.
Msigwa aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari wa mitandaoni na bloga katika kikao kazi kilicho andaliwa na Mamlaka ya
Mawasiliano Tanzania (TCRA) kilichofanyika Desemba 18, 2025 jijini Dar es
Salaam.
“Waandishi wa habari nchini siyo dhaifu kama wanavyosema
chukueni hatua ya kukabiliana nao kwa kuwajibu kulinda hadhi yenu msikae
kimya,” alisema Msigwa.
Alisema waandishi wa habari wa mitandaoni siyo dhaifu na kuwa
wanatekeleza wajibu wao ipasavyo na wana nafasi kubwa ya kutumia kalamu zao
kujenga nchi.
Msigwa aliwahakikishia waandishi ulinzi wa serikali, akisema
endapo sheria, kanuni au sera zitabainika kuwa kikwazo katika utendaji wao,
zitafanyiwa marekebisho kwa maslahi mapana ya taifa.
Msigwa alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuonesha
dhamira ya dhati ya kulea na kuwawezesha waandishi wa habari wa mitandaoni na
mabloga, badala ya kuwashughulikia kwa mtazamo wa adhabu, kujenga tasnia imara
na yenye tija ya habari nchini.
Aidha, Msigwa, aliipongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA) kwa mwelekeo wake wa kulea wadau wa sekta ya habari badala ya kuchukua
hatua kali za kinidhamu.
“ Mwelekeo huo unaendana na falsafa ya Serikali ya Awamu ya Sita
inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo inalenga kushirikiana na
wadau mbalimbali kwa manufaa ya taifa,” alisema.
Aliitaja Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jukwaa la Mitandao
Tanzania (JUMIKITA) kuwa ni wadau wakubwa wa serikali katika tasnia ya habari,
akisisitiza kuwa mchango wao ni muhimu katika kusambaza taarifa na kujenga
mawasiliano kati ya serikali na wananchi.
“Serikali imewaamini waandishi wa mitandaoni, sasa nanyi
muendelee kuonesha imani kwa serikali. Ushirikiano wetu umeendelea kuimarika na
changamoto zinazojitokeza tunazitatua kwa pamoja,” alisema Msigwa.
Alitangaza pia kuanza kwa maandalizi ya mafunzo kwa waandishi wa
habari kwa kushirikiana na TCRA, akiwataka kuyapokea kwa mtazamo chanya kama
sehemu ya kuongeza weledi na taaluma.
Kuhusu masuala ya kodi, Msigwa alisema serikali itaendelea
kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kutatua changamoto
zinazowakabili waandishi wa mitandaoni, akitambua mchango wao katika kuitangaza
nchi na kuvutia uwekezaji.
Aidha, alieleza kuwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ipo
katika mchakato wa kuanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kuwawezesha waandishi wa
habari, hususan wa mitandaoni.
Akizungumzia mazingira ya sasa ya kimataifa, Msigwa alisema vita
vya dunia ya sasa vimehama kutoka silaha za kijeshi kwenda kwenye taarifa,
akisisitiza kuwa vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda na kuipromote
nchi.
Aliwahimiza waandishi kuhakikisha majukwaa yao yanatumika
kulinda maslahi ya taifa na kuonya dhidi ya matumizi mabaya ya mitandao
yanayoweza kuharibu taswira ya Tanzania.
Hata hivyo, Msigwa alionesha kusikitishwa na tabia ya baadhi ya waandishi kunyamaza wanapodhalilishwa, akiwataka kusimama na kulinda hadhi ya taaluma yao.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, akisisitiza jambo kwenye kikao hicho.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabir Bakari, akizungumza kwenye kikao kazi hicho.
Meneja wa Huduma za Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mhandisi Andrew Kisaka, akizungumza.
Maafisa wa TCRA wakiwa kwenye kikao hicho
Mwendeshaji wa Blog ya Fullshangwe, John Bukuku akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Uchangiaji wa mambo kadha wa kadha ukiendelea.
Wanahabari wa mitandaoni wakiwa kwenye kikao hicho. Kutoka kushoto ni Frank Wandiba, Athuman Shomari na John Bukuku.
Blogers wakiwa kwenye kikao hicho. Kulia ni Mwendeshaji wa Blog ya Habari Faster, Emmy Mwaipopo.
Uchangiaji ukiendelea.
Mkurugenzi wa Magendela Blog, Hamisi Magendela (katikati) akiwa na Bloga wenzake kwenye kikao hicho.
Mwendeshaji wa Blog ya Kamanda wa Matukio, Richard Mwaikenda akichangia jambo kwenye kikao hicho.
kikao kikiendelea
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea
ohn Marwa kutoka Jambo online Tv akishukuru baada ya kutoa mchango wake kwenye kikao hicho.

Post a Comment